Na Munir Shemweta, MLELE

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Jimbo la Kavuu katika halmashauri ya Mpimbwe mkoa wa Katavi Mhe, Geophrey Pinda amekabidhi baiskeli za walemavu wa miguu ikiwa ni jitihada za kuwasaidia watu wenye ulemau.

Mhe, Pinda amekabidhi baiskali tarehe 2 Mei 2024 wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Kirida katika Kata ya Mamba halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele mkoa wa Katavi.

Baiskeli iliyokabidhiwa kwa mlemavu Bi. Adela John mkazi wa Kirida ni sehemu ya baiskeli nne zilizotolewa kwa walemavu wa miguu wa jimbo la Kavuu ikiwa ni njia ya kuwasaidia usafiri wa kuwawezesha kwenda maeneo mbalimbali.

Akizungumza wakati wa kukabidhi baiskeli hiyo, Mbunge wa jimbo hilo na Naibu Waziri wa Ardhi Mhe, Pinda amesema kuwa, anatambua adha wanayoipata walemavu wa miguu katika jimbo lake ndiyo maana ameona ipo haja ya kuwapatia baiskeli zitakazowasaidia kwenda katika shughuli zao.

‘’Ni matumaini yangu kuwa baiskeli hii itakuondolea adha uliyokuwa ukiipata na kwa sasa itakusaidia sana wakati wa kwenda katika shughuli zao mbalimbali’’ alisema Mhe, Pinda.

Mapema kwenye mkutano wake na wananchi wa kijiji cha Kirida katika kata ya Mamba halmashauri ya Mpimbwe wilayani Mlele mkoa wa Katavi, Mhe, Pinda aliwaeleza wananchi wa kijiji hicho kuwa, pamoja na kukabiliwa na majukumu ya uwaziri lakini amekuwa akifanya juhudi ya kuwatumikia katika kuwaletea maendeleo.

Amezitaja juhudi hizo kuwa ni pamoja na ujenzi wa barabara, zahanati na vituo vya afya, madaraja na shule za msingi na sekondari sambamba na upatikanaji huduma za umeme na maji.

‘’Pamoja na kwamba hamnioni mara kwa mara nikija hapa Kirida kutokana na majukumu niliyo nayo lakini nimekuwa nikifanya kazi kubwa ya kuwaletea maendeleo na haya maendeleo mnayo yaona kama vile ujenzi wa bararbara, shule, zahanati na vituo vya afya, zote ni jitihada ambazo ninazifanya’’. Alisema Mhe, Pinda.

Awali wananchi wa Kijiji cha Kirida katika kata ya Mamba walimueleza mbunge wa jimbo hilo kuwa wanakabiliwa na changamoto malimbali ikiwemo kutofanyika vikao vya kijiji kwa ajili ya kujua mapato na matumizi, kuwekewa alama za mipaka maeneo ya nyumba zao kwa madai kuwa makazi hayo yapo kwenye kingo ya mto na hivyo kutakiwa kuhama wakati mto ndiyo umehama.Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Jimbo la Kavuu katika halmashauri ya Mpimbwe mkoa wa Katavi Mhe, Geophrey Pinda (Kushoto) akimkabidhi Baiskeli Mlemavu wa Miguu Bi. Adela John wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Kidira katika kata ya Mamba halmashauri ya Mpimbwe mkoa wa Katavi Mei 2, 2024. Katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpimbwe Silas Ilumba.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Jimbo la Kavuu katika halmashauri ya Mpimbwe mkoa wa Katavi Mhe, Geophrey Pinda na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mpimbwe Silas Ilumba wakimuangalia Bi. Adela John ambaye ni mlemavu wa miguu mara baada ya kumkabidhi baiskeli tarehe 2 Mei 2024. 
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Jimbo la Kavuu Mhe, Geophrey Pinda akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kirida katika kata ya Mamba halmashauri ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakati wa ziara yake katika jimbo la Kavuu Mei 2, 2024.
Beda Andrea mkazi wa kijiji cha Kirida Kona akiwasilisha changamoto zake kwa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa jimbo la Kavuu Mhe, Geophrey Pinda (hayupo pichani) wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Kirida kata ya Mamba halmashauri ya Mpimbwe Mei 2, 2024.


Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Kirida katika kata ya Mamba halmashauri ya Mpimbwe wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Jimbo la Kavuu Mhe, Geophrey Pinda (Hayupo pichani) wakati wa mkutano wa hadahara uliofanyika kijiji cha Kirida Mei 2, 2024. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akikagua gwaride kabla ya kufunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akizungumza wakati alipofunga mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi la Ulinzi Tanzania Brigedia Jenerali Abubakari Charo akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Elias Sikaponda akizungumza wakati wa ufungaji wa mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba.
MKUU wa Kikosi cha Jeshi 838 JKT Maramba Kanali Ashraf Hassan akizungumza wakati wa mafunzo hayo.

Na Oscar Assenga, MKINGA.

MKUU wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda amesema mafunzo ya awali ya ya Kijeshi kwa vijana wa kujitolea Operesheni miaka 60 ya JKT kikosi cha Jeshi 838 Maramba huku akieleza umuhimu wa vijana hao ni mkubwa kutokana na kwamba wanaingia kwenye Jeshi la akiba ambalo inapotokea hitajiko la ulinzi wa Taifa wanaitwa kwa mujibu wa sheria.

Jenerali Mkunda aliyasema hayo Jumanne Aprili 30 mwaka huu wakati wa ufungaji wa mafunzo hayo ambapo aliwakilishwa na Brigedia Jenerali Abubakari Charo ambapo alisema kutokana na miongozo mbalimbali iliyopo kwa mafunzo hayo ya vijana hasa kwa kuzingatia kwamba vijana hao wanapohitimu mafunzo yao wanaingia kwenye jeshi la akiba.

Alisema kwamba linapotokea hitajiko la ulinzi wa Taifa na Rais na Amri Jeshi Mkuu akatangaza hali ya hatari vijana hao wanaitwa kwa mujibu wa sheria kwenda kuungana na Jeshi la Wananchi (JWTZ) kulinda ulinzi wa Taifa.

Aidha alisema kutokana na umuhimu wa vijana kwenye Jeshi hilo wanapenda kuona wanafikia viwango na malengo ya mafunzo hayo na amewaona wamefikia viwango vinavyotakiwa huku akieleza yanawajenga kwenye nidhamu, ukakamavu, uzalengo, uhodari wa kujiamini na kulipenda taifa lao.

“Nichukue fursa hii kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kutoa shukrani kwa dhati kwa Serikali kwa juhudi zinazofanyika kuhakikisha mazingira ya mafunzo kwa vijana ndani ya JKT yanaboreshwa”Alisema

“Kwani katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali imetoa kiasi cha sh Milioni 950 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni kwa vijana wanaojiunga na JKT fedha hizo zimeweza kujenga mabweni 12 kila moja lenye uwezo wa kuchukua vijana 120 hivyo kusaidia kikosi kuongeza uwezo kuchukua vijana 1440 na hii ni ishara za wazi kwamba serikali inatambua na kuthamini mafunzo ya vijana wa JKT”Alisema

“Lakini pia ujenzi wa vyoo vitano ambapo kila choo kina matundu 22 vitatumika kwa vijana hilo sio suala dogo ni jambo kubwa ambalo serikali imefanya kwa mazingira hayo wanawaomba vijana ambao hawapati fursa kujiunga na JKT wasije kufikiria wametengwa na kunyimwa fursa bali lengo vijana wote wapite Jkt na wale vijana wanaomaliza kidato cha sita”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Jeshi la Kujenga Taifa litakuwa likiendelea kuongozewa uwezo huku akieleza wanathamini juhudi za serikali katika kuboresha mazingira ya jeshi hilo ambapo mafunzo ambayo wameyapata yatawawezesha kuajiriwa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama,sekta mbalimbali za serikali au makampuni mbalimbali .

Awali akizungumza wakati akifunga mafunzo hayo Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian alisema mafunzo hayo kwa vijana wa JKT ni muhimu sana kwa vijana kwa maana wao ndio tegemeo la Taifa.

Balozi Batilda alisema Rais Dkt Samia Suluhu kupitia falsafa yake ya 4R ameendelea kusimamia na ndio maana juzi chadema walikuwa na maandamano yao wakasimamiwa vizuri na jeshi la Polisi wakafanya mkutano wao wakatembea.

Alisema kwa hakika wakawa na matumaini watapata mambo ya msingi yatakayowasaidia kujenga nchi lakini wakasikia mambo tofauti kwanini wakuu wa mikoa hawapigiri kura, kama madiwani sasa akasema hata RC akipigiwa kura atachaguliwa Tanga na RC ni msaidizi wa Rais anaweza kuhamishwa kila eneo.

“Tulitegemea kwamba hivi sasa nchi ipo kwenye kipindi kigumu na mvua zinanyesha madhara maeneo mengi barabara nyingi zimepata changamoto na maeneo mengi lami zimepasuka changamoto ni nyingi vita vya israel vinaendelea duniani gharama zinapanda bei ya dola ipo kubwa kulingana na bei yetu sisi tukaona haja hoja zao za za kwamba hazikuwasaidia wakapata mawazo mbadala hazipo"Alisema.

Hata hivyo Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Elias Sikaponda alisema kwamba alisema mafunzo hayo ni muhimu kwa sababu yanaleta tija kwa vijana katika shughuli za kujitegemea huku akiwataka kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya.

Aliwataka pia vijana hao kutumia elimu waliyoipata wakaweze kutatua changamoto mbalimbali pasipo kuvunja sheria na taratibu zilizowekwa hapa nchini huku akisiistiza watumie nidhamu pekee kama silaha kwenye jambo lolote mbeleni.


Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetangaza kuwa uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kwahani lililopo Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar utafanyika tarehe 08 Juni, 2024.

Taarifa kwa umma iliyotolewa na kusainiwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Bw. Kailima, R. K jijini Dodoma leo tarehe 02 Mei, 2024 imesema kwamba fomu za uteuzi kwa ajili ya uchaguzi huo mdogo zitatolewa kuanzia tarehe 17 hadi 23 Mei, 2024.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa uteuzi wa wagombea utafanyika tarehe 23 Mei, 2024 na kampeni kwa ajili ya uchaguzi huo zitafanyika kuanzia tarehe 24 Mei, 2024 hadi tarehe 07 Juni, 2024.

Tume imetangaza uchaguzi huo mdogo kufuatia taarifa ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iliyomtaarifu Mwenyekiti wa Tume kuhusu uwepo wa nafasi wazi ya ubunge katika Jimbo la Kwahani.

Spika ametoa taarifa hiyo kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 49(2) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka, 2024.

“Kwa kuzingatia matakwa ya kifungu cha 49(1)(b) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024, Tume inatoa taarifa kwa umma kuhusu uwepo wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Kwahani lililopo Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Tume imevikumbusha vyama vya siasa, wagombea na wadau wote wa uchaguzi kuzingatia Katiba, sheria, kanuni, maadili ya uchaguzi, taratibu, miongozo na maelekezo ya Tume katika kipindi cha uchaguzi huo mdogo.

Dar es Salaam. Maeneo tofauti nchini Tanzania yanashuhudia mvua kubwa ambazo sio tu zinaathiri miundombinu na kuhatarisha usalama wa maisha ya watu bali pia inaweza kuwa hata kwa vifaa vya umeme nyumbani.

Watu wengi huingia hasara wakati vyombo vyao vya umeme walivyovinunua kwa gharama kubwa kuharibika kutokana na hitilafu za umeme. Mara nyingi matukio ya aina haya yanaweza kuzuilika endapo tahadhari zikichukuliwa mapema.

Akizungumzia kuhusu mambo muhimu ya kuzingatia, Meneja wa Bidhaa za Kieletroniki wa Samsung Tanzania, Bw. Evans Songa ametolea ufafanuzi maswali ya msingi ambayo wateja wengi wamekuwa nayo hususani kwa wanaoishi na familia au wenyewe, ili kuhakikisha usalama wa vyombo vya umeme nyumbani.

Swali: Kuna hatari zipi za kushika vyombo vya umeme kwa mikono ikiwa na maji?

Jibu: Bila shaka wote tunafahamu kwamba maji na umeme haviendani. Madhara ya kutumia vyombo vya umeme mikono ikiwa imelowana ni pamoja na mtumiaji kupigwa shoti ya umeme. Pia, unaweza kusababisha shoti kwenye kifaa chako. Kuna baadhi ya vifaa vinakuelekeza uhakikishe kuwa ni vikavu kabla ya kuchomeka katika soketi ya umeme.

Swali: Nini kinashauriwa baada ya kumaliza matumizi ya vyombo vya umeme nyumbani?

Jibu: Kuna baadhi ya watu wana kawaida ya kuacha vyombo vyao katika soketi za umeme baada ya kumaliza matumizi. Mbaya zaidi wengine husahau hata kuzima kabisa kutokana na vifaa vingi vya siku hizi ni automatic hivyo kujizima vyenyewe mara tu vikimaliza kazi iliyokusudiwa. Tabia hii inaongeza hatari ya chombo kuharibika au kuungua endapo kutatokea shoti ya umeme. Umeme kujizima na kujiwasha hususani kipindi hiki cha mvua ni kawaida hivyo unashauriwa ni vema kuzima na kuchomoa chombo chako katika soketi ya umeme baada ya kumaliza matumizi. Hii itakulinda hata endapo utatoka nyumbani kwako kwa dharura au kuendelea shughuli zingine.


Swali: Kuna faida gani ya kusafisha vyombo vya umeme mara kwa mara baada ya kumaliza matumizi?

Jibu: Inashauriwa kusafisha vyombo vyako vya umeme mara tu baada ya kumaliza matumizi. Hii itakusaidia kulinda vyombo vyako hususani kwa kuvieupusha na mazingira ambayo yanaweza kuleta kutu. Ukiachana na kusafisha pia hakikisha unakuwa unavitumia vyombo vyako mara kwa mara ili kujua kama vinafanya kazi kwa ufasaha au la. Sidhani kama utafurahi siku ambayo una uhitaji zaidi wa chombo chako na kugundua kuwa hakifanyi kazi aidha kutokana na kutokitunza au kujaribu kama kinafanya kazi mara kwa mara.

Swali: Kuna umuhimu gani wa kuwa na warantii kwa vyombo vya umeme?

Jibu: Kwanza kabisa, kwa wasiofahamu warantii ni dhamana ya muda maalumu inayotolewa kwa ajili ya matazamio ya bidhaa ili kumhakikishia mtumiaji juu ya ubora na ufanyaji kazi wa bidhaa husika. Sio kampuni zote zinatoa warantii kwa bidhaa wanazouza kwa wateja wake. Lakini kuna makampuni ambayo yanazingatia hili ili kuwaridhisha na kuwapatia amani wateja wake dhidi ya hofu ya vyombo vyao pindi vikipata hitilafu. Kwa mfano, Samsung hutoa warantii kwa bidhaa zake kwa muda wa miaka miwili na miaka 20 kwa bidhaa zenye kompresa na mota. Bidhaa hizo ni pamoja na runinga, majokofu au friji, mashine za kufulia, kupashia chakula, kiyoyozi, nakadhalika.

Ukiachana na warantii, pia humhakikishia mteja kupata huduma kutoka kwa wataalamu wao wenye weledi, huduma kwa mteja ya uhakika, vifaa halisi marekebisho yakihitajika, pamoja na kupokea taarifa za mara kwa mara kuhusu kifaa husika. Kigezo muhimu cha kupata warantii ni kununua bidhaa kutoka kwa mawakala wa bidhaa waliohakikiwa pamoja na kuwa na kadi ya warantii kwa bidhaa za nyumbani.

Kwa kumalizia, familia nyingi zinatumia vyombo vya umeme nyumbani kutokana na maendeleo ya kiuchumi yanayochochewa na uvumbuzi katika sekta ya sayansi na kiteknolojia. Kuongezeka kwa makampuni ya utengenezaji na usambazaji wa vifaa hivyo pia kumepelekea urahisi na unafuu wa upatikanaji wake. Bila kusahau kuongezeka kwa matumizi ya umeme nchini kote ambayo yanahamasisha watu kubadilika kuendana na wakati. Hivyo, ni muhimu kuchukua hatua kila mara unapokuwa haupo nyumbani kwa usalama wa vyombo vyako, wewe mwenyewe na uwapendao.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi (wa pili kushoto) na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais ,Mary Maganga (wa pili kulia) wakikabidhi tuzo ya ushindi wa Jumla kwa wafanyakazi wa Barrick (kutoka kushoto) ni Hassan Kallegeya Safety Coordinator (Bulyanhulu) na kulia ni Aristides Medard (Specialist Occupational Hygiene, Katika hafla iliyofanyika jijini Arusha. Mbali na ushindi wa Jumla Barrick imeshinda tuzo nyingine 4
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nicolaus Mkapa, akimkabidhi tuzo kwa ushindi wa kwanza katika sekta ya madini kwa Mtaalamu wa masuala ya Usalama wa Barrick –Specialist Occupational Hygiene, Aristides Medard katika hafla ya kukabidhi tuzo iliyofanyika jijini Arusha. Wengine pichani ni Wafanyakazi wa Barrick. Mbali na ushindi wa Jumla Barrick imeshinda tuzo nyingine 4.
Wafanyakazi wa Barrick wakifurahia tuzo ambazo kampuni imejishindia.

Na Mwandishi Wetu.

Barrick Tanzania imenyakua tuzo tano katika hafla ya utoaji wa tuzo za Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ya 2024 iliyofanyika jijini Arusha ambapo Mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu, umeshinda tuzo kubwa ya mshindi wa juu wa Jumla katika Tuzo ya Afya na Usalama (OHS) 2024.

Mbali na ushindi huo mkubwa, Bulyanhulu, pia ilinyakua tuzo za Utawala Bora ofisini, usaidizi wa kiofisi na shughuli za ukuzaji biashara , na mshindi Bora wa Ubunifu kwenye maonyesho ya OSHA ya mwaka huu kwenye sekta ya madini.

Kwa upande wake, Barrick North Mara ilishinda tuzo ya juu katika Kuwajali Zaidi Wafanyakazi wenye Mahitaji Maalum.

Maonyesho ya OSHA mwaka huu yalifanyika katika viwanja vya General Tyre jijini Arusha, ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu, Mhe. Deogratius Ndejembi katika hafla ya utoaji wa tuzo za mwaka huu ambapo aliwakilishwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Patrobas Katambi.

Barrick Tanzania imeshinda tuzo za 2024 kutokana na mafanikio ya 2023 ya kampuni ambapo ilishinda tuzo ya jumla ikiwemo tuzo za uandaaji Ripoti Bora ya Tathmini ya Hatari katika uchimbaji madini na mshindi Bora wa tuzo ya Usalama na afya (OHS) katika sekta ya madini.

Tuzo nyingine ilizoshinda zilikuwa ni Kujali zaidi Wafanyakazi wenye Mahitaji Maalum na utekelezaji sera bora ya Usalama mahali pa kazi (OHS), mshindi wa pili kwa washindi wa jumla wa sekta ya Madini, utekelezaji Mpango Kazi Bora wa Usalama na Afya mahali pa kazi.

Usalama ni sehemu muhimu ya DNA ya Barrick. Kampuni ina mpango maalum kwa ajili ya usalama wa wafanyakazi wake na wakandarasi, kuhakikisha kwamba kila mtu anarudi nyumbani akiwa na afya njema na salama. Juu ya yote hayo katika Barrick kila mtu amejitolea kufanya a kuhakikisha hakuna matukuo ya ajali katika sehemu yake anapofanyia kazi.

Katika maonesho ya mwaka huu Barrick pia ilifiikisha elimu ya afya na usalama kwa wananchi waliotembelea kwenye banda lake kwenye maonesho haya sambamba na kushiriki zoezi la kupanda miti katika kutekeleza kwa vitendo kauli mbiu ya maonesho ya athari za mabadiliko ya tabia nchi katika usalama na afya kazini:sajili eneo lako la kazi OSHA katika harakati za kupunguza athari hizo.
Baadhi ya Watumishi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) wakisherehekea Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani, kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha wakipita mbele ya jukwaa kuu.
Baadhi ya Watumishi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) wakiwa katika maandamano ya Kuingia katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha ambapo Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yanafanyika Kitaifa.
Baadhi ya Watumishi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) wakiwa katika Picha ya Pamoja wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambapo kitaifa yanafanyika jijini Arusha.
Baadhi ya Watumishi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) wakiwa katika Picha ya Pamoja wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ambapo kitaifa yanafanyika jijini Arusha
-----
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) leo tarehe 1 Mei, 2024 imeungana na Watanzania kote nchini kusherekea siku ya Wafanyakazi Duniani, maarufu kama Mei Mosi.

Sherehe hizo ambazo zimefanyika kitaifa jijini Arusha katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Kitaifa huku mgeni rasmi akiwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Philip Isdor Mpango.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo akizungumza katika kongamano la uwekezaji kwenye sekta ya Utalii Jijini Arusha Leo 30 April 2024Mkurugenzi Mtendaji kituo cha uwekezaji Tanzania TIC Bw. Gilead Teri akizungumza na katika kongamano la uwekezaji katika Ukumbi wa mkutano Gran Melia Jijini Arusha, Aprili 30, 2024.
Waziri wa Maliasili na Utalii Angela Kairuki akizungumza kwenye kongamano la sekta ya Utalii katika mkoa wa Arusha 30 April 2024
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda akiwakaribisha wageni waliokuja kwenye kongamano la uwekezaji kwenye sekta ya Utalii mkoa wa Arusha leo 30April, 2024. 
Washiriki wa kongamano la uwekezaji wa Utalii lililofanyila leo 30april 2024 Katika hotel ya Garan Melia Jijini Arusha
Washiriki wa kongamano la uwekezaji wa Utalii lililofanyila leo 30april 2024 Katika hotel ya Garan Melia Jijini Arusha

Na Vero Ignatus, Arusha.

Kituo cha uwekezaji (TIC) kinatarajiwa kujengwa mkoani Arusha ikiwa ni kuondoa urasimu wanaokutana nao wawekezaji ili kupata hati na nyaraka zote kwa wakati katika kituo cha pamoja kwa lengo la kuinua uchumi.

Hayo yamesemwa leo Jijini Arusha na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo wakati akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Kongamano la Uwekezaji kwenye Sekta ya Utalii lililohudhuriwa na zaidi ya wadau 420 kutoka Serikalini, wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.

Prof. Mkumbo ameeleza kuwa kupitia utekelezaji wa sera na sheria mbalimbali za uwekezaji na maelekezo mahususi ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali imeendelea kupata mafanikio mbalimbali katika kuhamasisha, kuvutia na kuwezesha uwekezaji nchini.

Prof. Mkumbo ameainisha mambo 10 ya msingi katika utalii ikiwemo Amani, Utulivu na Salama, Malazi miundombinu ya usafiri, Mikakati mizuri ya kutangaza Utalii, Suala la tabia njema na ukarimu wa wenyeji, uwepo wa miundombinu ya malazi, Elimu kwa watoaji huduma kwa watalii, uwepo wa mitaji kwaajili ya uwekezaji , uwepo wa idadi ya watu wenye uwezo wa kuongea lugha zaidi ya moja, kuwepo na vituo vya kujifunza lugha. na Uhusiano bora wa kimataifa

Akizungumza katika kongamano hilo Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Angela Kairuki (Mb) amesema kutoka na Royal tour wameweza kufikia watalii mil 1.8 na wanajianda zaidi kuona namna ya kuongeza watalii na maeneo ya malazi ikiwemo kuandaa malazi ya madaraja mbalimbali yenye ubora, usafi pamoja na huduma zinazopatikana.

"Fursa bado zipo katika mnyororo wa thamani ambapo kwa umoja wetu utatusaidia kuboresha uchumi zaidi na kuongeza Pato Ila Lengo likiwa ni kuvuka matarajio watalii wanapokuja wapate kumbukumbu nzuri sambaba na wenyeji wasiwe ndugu watazamaji badala yake na wawe wa moja katika kuongezea pato la Taifa".

"Tunatakiwa kuongeza Utalii wa mikutano kwa kuhakikisha ukumbi huo wa AICC unakamilika kwa haraka Uwe na Tija ili wageni waweze kuvutiwa zaidi pamoja na kuliongezea Taifa kipato", Alisema.

Akieleza Maudhui ya mkutano huu Dkt. Tausi M Kida katibu mkuu ofisi ya Rais mipango na uwekezaji amesema kongamano hilo ni takwa kutoka ktk ofisi hiyo ambayo Mh. Rais aliitoa wakati akiwaapisha viongozi

Aidha amesema kuwa Utalii wa ndani unaongezeka kwa kasi hadi kufikia 1.9 mil tofauti na hapo awali, kwani mwaka 2022 Tanzania ilikuwa inapokea watalii 1.5 milioni ukilinganishwa na make 2023 watalii wameongezeka hadi kufikia million 2 amesema kwa sasa Tanzani inapokea wageni mil 4 huku changamoto ya vidanda ikiwepo132, 676

Dkt. Kida ameweza kuainisha Malengo ya kongamano hilo Kufahamu Fursa za biashara zilizopo ikiwa ni pamoja
Kufahamu mwenendo wa Fursa za Utalii na mwenendo wa Utalii nchini
Fursa za ushirikiano kupitia ofisi ya msajili wa hazina, Fursa ya kutbua na kubaini mikakati kuboresha huduma za Utalii nchini sambaba na kuongeza vitanda kwaajili ya wageni wanaoingia nchini

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Christian Makonda ni ombi letu kwamba Arusha kuwepo na one stop Centre kwamba mgeni anapofika aweze kuondoka na certificate yake, vile vile mkoa huu unaochangia Pato la Taifa kwa kuingiza fedha za kigeni hivyo tutahakikisha Arusha inakiwa na umeme wa kutosha

"Tunataka kamera ziwepo kila eneo la mji wa Arusha, ifikapo mwezi Julai mwaka huu Taa na watu wanafanya shughuli zao ni la kubughudhiwa, Barabara zetu mkoa wa Arusha ni mbovu na ni aibu kubwa labda nimuulize Dada yangu Angela Kama wameamua barabara hizi ziwe kivutio cha watalii sawa Sisi hatuna tatizo tutarendelea kupromote la sivyo tupeni pesa kwaajili ya kutengeneza barabara "Tumekubaliana na Tanrod tunakwenda kuondoka mabango yote Arusha na tunaweka eletronic"

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha uwekezaji (TIC) Bw. Gilead Teri amesema kuwa katika uwekezaji wa kukuza na kuimarisha Sekta ya Utalii nchini, Serikali ya awamu ya sita imeweka mikakati mbalimbali ili kuhakikisha, wananchi wanafanya uwekezaji mkubwa kwenye sekta hiyo, ikiwa ni pamoja na kutoa msamaha wa ushuru na punguzo la kodi kwa wawekezaji.

Teri amesema kuwa, kutokana na ongezeko la idadi ya watalii inayotokana na programu ya Tanzania Royal Tour iliyofanywa na Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan mwaka 2022, imeandaa Sera inayolinda mtaji wa Mwekezaji kwa kushusha kodi kutoa dola 1,000 mpaka kufikia laki 5 na dola elfu 50 kwa wazawa huku ikitoa msamaha wa ushuru mpaka pale mtaji utakapoanza kutoa faida.

"Tunataka mtaji wa Mwekezaji utumike kukuza mtaji wake badala ya kulipa mrundikano wa kodi, na kuruhusu kuanza kulipa kodi mara baada ya kutengeneza faida, hali ambayo licha ya kutoa unafuu kwa wawekezaji inasaidia kuvutia wawekezaji wengi zaidi wazawa na wageni kuwekeza kwenye sekta ya Utalii" Amesema Terry

Aidha, ameyataja malengo ya Kongamano hilo ni pamoja na kuwajulisha wadau fursa zinazopatikana kwenye sekta ya utalii na nafuu mbalimbali zilizowekwa na Serikali kupitia sheria ya Uwekezaji ya mwaka 2022 na kusisitiza wawekezaji kuwa huu ni mwaka wa kutengeneza faida kupitia sekta hiyo.

Amefafanua kuwa, Kongamano hilo litatoa fursa ya kuwasilisha fursa, zinazopatikana kwenye sekta ya utalii, mawasilisho yatakayochochea majadiliano kati ya watalamu na wadau waliopo kwenye sekta ya Utalii mkoani Arusha, ili kujua fursa na changamoto zilizopo ili kuongeza kiwango cha uwekezaji kwenye sekta hiyo.

Aidha Kongamano hilo limeanyika kufuatia maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoyatoa wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali mwanzoni mwa mwezi Aprili, 2024, akimtaka Mkuu wa Mkoa wa Arusha, kushughulikia changamoto ya upatikanaji wa vyumba vya kulala wageni wanaotembelea Mkoa wa Arusha

Kongamano hilo limebeba "Kauli Mbiu ya Uwekezaji Katika Utalii Endelevu, Uchangamkiaji wa fursa za Uwekezaji baada ya Program ya Tanzania 'The Royal Tour'.
Na Oscar Assenga, KOROGWE.

KAMPENI ya Usalama barabara inayotolewa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana an Shirika la Amend Tanzania kupitia Ubalozi wa Uswis nchini imewafikia waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda eneo la Hale wilaya ya Korogwe huku ikielezwa zaidi ya waendesha Bodaboda kati ya 5 mpaka 10 wanapoteza maisha kwa siku katika Mkoa wa Tanga kutokana na ajali za barabarani.

Chanzo kikubwa kikitajwa ni kuchangia wa na kutokuzingatia sheria za usalama wanapokuwa wakiendesha vyombo vya moto pamoja na kuendesha mwendokasi.

Hayo yalisemwa na Kaimu Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga (RTO) Hamis Mbilikila wakati wa utoaji wa elimu katika kampeni ya usalama barabarani iliyokuwa ikitolewa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Shirika la Amend kupitia ufadhili wa Ubalozi wa Uswis Tanzania iliyofanyika Hale wilayani Korogwe .

Hali hiyo inachangia kwa asilimia kubwa kupelekea kupoteza nguvu kazi kubwa ya vijana kutokana na asilimia kubwa kujiajiri kupitia sekta hiyo bila kuwa na elimu ya sheria za usalama barabarani wakati wakitekeleza majukumu yao ya kila siku.

Alisema ajali hiyo zinatokana na asilimia kubwa kutokuzingatia sheria za usalama barabarani hivyo uwepo wa mafunzo hayo ambayo yanatolewa na Shirika hilo kwa mkoa huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali zinazotokana na madereva hao wa pikipiki maarufu kama bodaboda.

Aidha alisema kwamba mafunzo hayo wanaamini yatakuwa na tija ka madereva hao ambao huku akiwataka pia kuacha kujichukulia sheria mkononi pindi ajali zinazopotekea kweye maeneo yao badala yake watoe taarifa kwenye mamlaka husika.

“Ndugu zangu bodabda ajali zinapotkea msijichukulie sheria mkonono mtoe taarifa mkoa wa Tanga ni wa kimkakati tumeona mambo mengi yanafanyika kuna bomba la mafuta kuna wageni wengi Bandari yetu imefunguka kuna njia inaunganisha nchi jirani na Kenya na hapa hale ni barabara kuu kuna watu wengi wanapita hivyo ni lazima tufuate sheria za usalama barabara”Alisema

Aidha aliwataka waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda kuacha kujichukulia sheria za usalama barabarani kutokana na kwamba hawawezi kujua watakumbana na jambo gani lakini pia madhara ya ajali ni kupoteza maisha na vifo .

“Vijana wengi wanapoteza maisha kupitia vyombo hivyo pikipiki zimekuja kutusaidia na asilimia kubwa kwenye vijiji pikipiki ni muhimu hivyo kutokana na adhari hivyo Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Shirika la Amend kwa ufadhili wa Ubalozi wa Uswis wameona wawape mafunzo hayo ili tuweze kujua sheria za usalama barabarani”Alisema

Awali akizungumza katika mafunzo hayo Afisa Miradi kutoka Shirika la Amend Tanzania Scolastica Mbilinyi alisema lengo lao ni kupeleka mafunzo kwenye maeneo mbalimbali ili kuwafikia watu wengi sana kwenye kampeni ya usalama barabarani na sasa wanayafikia maeneo ya pembezoni ambao ni mpango kazi wa dunia kupunguza ajali angalau kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.

“Tulianza wilaya ya Tanga na baadae Mkanyageni wilaya ya Muheza walianza leo tupo Hale wilaya ya Korogwe na tumepanga kupeleka elimu hii kwenye maeneo mengi kwa sababu wengi hawana elimu ya usalama barabarani na itasaidia kuokoa maisha ya watu wengi zaidi baada ya kupata elimu hii”Alisema

Afisa Mradi huyo aliwataka bodaboda wafuata sheria za usalama barabarani ikiwemo wahakikishe wanatembea spidi inayotakiwa na sehemu kwenye matuta waweze kupunguza mwendo ikiwemo kuhakikisha pikipiki walizokuwa nazo zimekamilika kwa sabababu itawasaidia kupunguza ajali kwa asilimia kubwa .

“Lakini sisi tunatoa elimu ya usalama barabarani kwa shule za Sekondari,Msingi na kwenye Jamii pamoja na madereva wa pikipikimaarufu kama bodabda na tumekua tukishirikiana na Jeshi la Polisi na mafunzo hayo yanaratibiwa na Jeshi hilo”Alisema

Naye kwa upande wake Mratibu wa Shirika la Amend Tanzania Ramadhani Nyanza –aliwashukuru  bodaboda kwa mwitiko mzuri wao waliojitokeza kwa wingi huku akieleza mikakati yao baada ya kutoka Hale watakwenda Korogwe,Mombo, Segera, Handeni na Kilindi kwani hilo ni kundi kubwa lipo kwenye hatari kwa ajali ni bodaboda.

“Barabara zetu mnaziona kila siku mnaingia barabarani hakuna njia za waendesha pikipiki ni hiyo hiyo moja kisheria kama kuna sehemu wanatembea 50 nao wanatembea hivyo hivyo wanapiga honi muwapishe kwa hiyo mkijiweka kwenye hali ya kudharaulika na watu wanawafanya hivyo wao mnapoamua kuwatoa huko ni kampeni ya usalama barabarani hao wakiwa salama askari watakuwa salama na abiria wao”Alisema

Akizungumza na mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Isa Juma ambaye ni bodaboda kituo cha Hale alisema wanashukuru wamepata elimu hiyo nzuri na kuna mambo mengi wamejifunza ambayo watayatumia ili kuondokana na ajali za barabarani.

Alisema pia mafunzo hayo yamewapa mwanga wa kuona namna nzuri ya kutumia sheria za usalama barabarani kwani kuna vitu vingi walikuwa hawavijui na wameelezwa hivyo vitakuwa chachu kwao kuepukana na ajali .